Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Benki ya Dunia Yatoa Ufadhili wa Shilingi Bil. 47 Kuhifadhi Rasilimali ya Bonde la Mto Wami - Ruvu.
Jan 20, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_27493" align="aligncenter" width="815"] Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe akisisitiza umuhimu wa Kutunza mazingira ili kulinda vyanzo vya maji wakati wa uzinduzi wa mradi wa uhifadhi wa rasilimali maji awamu ya pili wa Wami- Ruvu Basin utakaotekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia uliofanyika mapema leo Mjini Dodoma ambapo alikuwa mgeni rasmi.[/caption]

Na. Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.

Benki ya Dunia imetoa ufadhili wa shilingi Bilioni 47 kutekeleza mradi wa uhifadhi wa rasilimali za maji awamu ya pili katika bonde la mto Wami.

Akizindua mradi huo mapema leo, Mjini Dodoma Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe amesema kuwa Tanzania ina jumla ya mabonde tisa ya maji lakini mabonde hayo yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na shughuli za kibinadamu na kiuchumi zinazosababisha kupungua kwa maji katika mabonde hayo.

[caption id="attachment_27494" align="aligncenter" width="750"] Mkurugenzi wa Ubora wa Maji Bibi Nadhifa Kennikimba akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji wakati wa uzinduzi wa mradi wa uhifadhi wa rasilimali maji awamu ya pili wa Wami- Ruvu Basin utakaotekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia, kushoto ni . Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe.[/caption] [caption id="attachment_27495" align="aligncenter" width="750"] Mtaalamu wa masuala ya Usimamizi wa rasilimali maji kutoka Benki ya Dunia Dkt. Jacqueline Marie Tront akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa uhifadhi wa rasilimali maji awamu ya pili wa Wami- Ruvu Basin R utakaotekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia[/caption]  

"Fedha hizi zilizotolewa na Benki ya Dunia zitaenda kutoa elimu kuanzia ngazi ya juu mpaka mwananchi wa kawaida juu ya njia za kutumika kutunza rasimalimali za maji ndani ya hifadhi ya bonde la mto Wami," alisema Mhandisi Kamwelwe.

Aidha Mhandisi Kamwelwe amewataka wananchi na viongozi watakaopata elimu hiyo kutunza   rasilimali hiyo wao wenyewe kwa kutofanya shughuli za kibinadamu na za kiuchumi ndani ya hifadhi la bonde hilo.

[caption id="attachment_27496" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe( Katikati) akizindua mpango wa mradi wa uhifadhi wa rasilimali maji awamu ya pili wa Wami- Ruvu Basin utakaotekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia[/caption] [caption id="attachment_27497" align="aligncenter" width="750"] Muwakilishi wa Benki ya Dunia Bw. Alex William akizungumzia namna Benki ya Dunia inavyosaidia miradi ya maji hapa nchini ambapo kwa sasa imetoa bilioni 47 kwa ajili ya mradi wa kuhifadhi rasilimali maji awamu ya pili wa Wami- Ruvu Basin.[/caption] [caption id="attachment_27498" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe( Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Washiriki wa uzinduzi wa mradi wa uhifadhi wa rasilimali maji awamu ya pili wa Wami- Ruvu Basin utakaotekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia[/caption] [caption id="attachment_27499" align="aligncenter" width="750"] Washiriki wa uzinduzi wa mradi wa uhifadhi wa rasilimali maji katika Bonde la mto Wami Ruvu utakaoteklezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia wakifuatilia Hotuba ya mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi. Isack Kamwelwe. (Picha zote na Frank Mvungi)[/caption]

Kwa upande wake, mwakilishi wa Benki ya Dunia Alex William amesema kuwa jukumu la utunzaji wa rasilimali za maji ni za kila mwananchi, kiongozi pamoja na taasisi za umma na binafsiHivyo amewata Watanzania kupitia mradi huo kutunza rasilimali hiyo ili kuongeza kiwango cha maji ndani ya bonde hilo ambayo yatatumika katika shughuli za nyumbani, viwandani, mashambani katika shughuli za uvuvi pamoja na utalii.

​  

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi