Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

“Nchi Yetu iko Salama dhidi ya Corona” – Dkt. Abbasi
Mar 15, 2020
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_51619" align="aligncenter" width="750"] Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiongea na waandishi wa habari, leo Machi 15, 2020 Jijini Dodoma[/caption] [caption id="attachment_51618" align="aligncenter" width="750"] Waandishi wa habari wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi wakati wa mkutano alioufanya leo Machi 15, 2020 Jijini Dodoma[/caption]

Na. Immaculate Makilika - MAELEZO

Serikali imesema nchi iko salama dhidi ya ugonjwa wa CORONA  na tayari imechukua hatua kadhaa za tahadhari ili kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa huo hapa nchini.

Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari leo jijini Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi amesema kuwa, Serikali imeendelea kufanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha kwamba ugonjwa huo sio tu hauingii nchini, lakini pia kuzuia kusambaa kwa maambukizi endapo utaingia.

“Zipo hatua zinazochukuliwa ndani ya Taasisi na Wizara moja moja, lakini pia zipo hatua za kitaifa za kukabiliana na ugonjwa huu, na hivyo naomba kuwatoa hofu watanzania kuhusu ugonjwa huu” alisema Dkt. Abbasi

Akifafanua hatua ya kwanza ya kukabiliana na ugonjwa huo, Dkt. Abbasi alisema, Serikali imeandaa utaratibu maalum katika maeneo ya Viwanja vya  ndege na maeneo ya mipakani, ambapo watu hawapimwi ugonjwa  wa corona bali joto la mwili ili kuangalia endapo joto limezidi kiwango cha kawaida  cha binadamu.

“Watanzania waendelee kuchukua tahadhari kama Rais Magufuli alivyoeleza na wazingatie maelekezo ya namna ya kujikinga yanayoendelea kutolewa na Wizara ya Afya kupitia wataalamu  wake” alisema Msemaji wa Serikali

Dkt. Abbasi amefafanua kuwa  katika hatua ya pili, Serikali imeandaa  vituo maalum vya kuwatenga washukiwa, na kuna vifaa vyote vya kupima huu ugonjwa. Aidha, hatua ya tatu ni kuwepo kwa hospitali maalum katika kanda zote nchini, ambazo zimetengwa  na zitatangazwa endapo atatokea mgonjwa wa CORONA.

Vilevile, Serikali inaendelea  kufanya jitihada  katika kupambana na ugonjwa huo  ikiwemo kusitisha safari za ndege katika nchi za China na Italia na safari ya timu ya Taifa ya mpira wa miguu iliyokuwa iende nchini Tunisia kwa ajili ya mchezo uliokuwa ufanyike hivi karibuni .

Dkt. Abbasi amevipongeza Vyombo vya Habari nchini kwa kuitikia wito wa Rais wa kuhabarisha umma kuhusu ugonjwa huu, na kuwataka kuzingatia maelekezo ya wataalamu.

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi