Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Matukio Katika Picha Kufungwa Kwa Mafunzo ya WISN na POA Jijini Mbeya
Jun 08, 2018
Na Msemaji Mkuu

Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Utawala na RasilimaliWatu Mkoa wa Katavi Bi. Crescencia Joseph akifunga mafunzo ya mifumo  ya WISN na POA, Mifumo  hiyo inatumika kubaini mahitaji ya watumishi katika vituo vya kutolea huduma za afya na vipaumbele katika kuwapangia watumishi hao vituo vya kazi , mafunzo hayo yanayowashirikisha makatibu wa afya,maafisa utumishi,wataalamu wa takwimu za afya na waganga wakuu wa Wilaya za mkoa wa Katavi leo Jijini Mbeya.

Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Utawala na RasilimaliWatu Mkoa wa Katavi Bi. Crescencia Joseph akimkabidhi Afisa Utumishi na Utawala wa Halmashuri ya Wilaya ya Nsimbo Bw. Betueli Ruhega Kiongozi cha Utaratibu wa Mafunzo elekezi ya Awali kwa Watumishi Wapya wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, wakati wa hafla ya kufunga mafunzo yanayowashirikisha makatibu wa afya, maafisa utumishi, wataalamu wa takwimu za afya na waganga wakuu wa Wilaya za mkoa wa Katavi leo Jijini Mbeya.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya matumizi ya mfumo wa WISN na POA yaliyofungwa leo  ambapo yaliwshirikisha makatibu wa afya,maafisa utumishi, wataalamu wa takwimu za afya na waganga wakuu wa Wilaya za mkoa wa Katavi leo Jijini Mbeya.

Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Utawala na RasilimaliWatu Mkoa wa Katavi Bi. Crescencia Joseph (katikati) akionesha Kiongozi cha Utaratibu wa Mafunzo elekezi ya Awali kwa Watumishi Wapya wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, wakati wa hafla ya kufunga mafunzo yaliyowashirikisha makatibu wa afya, maafisa utumishi, wataalamu wa takwimu za afya na waganga wakuu wa Wilaya za mkoa wa Katavi leo Jijini Mbeya.

Afisa Utumishi na Utawala wa Halmashuri ya Wilaya ya Nsimbo Bw. Betueli Ruhega akisoma Kiongozi cha Utaratibu wa Mafunzo elekezi ya Awali kwa Watumishi  Wapya wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, wakati wa hafla ya kufunga mafunzo yaliyowashirikisha makatibu wa afya, maafisa utumishi, wataalamu wa takwimu za afya na waganga wakuu wa Wilaya za mkoa wa Katavi leo Jijini Mbeya.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia hotuba ya Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Utawala na RasilimaliWatu Mkoa wa Katavi Bi. Crescencia Joseph wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo  leo  Jijini Mbeya.

            (Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO, Mbeya)

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi