Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Aug 28, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_10681" align="aligncenter" width="776"] Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bibi Rehema Madenge akifungua mafunzo kwa watumiaji wa Mfumo mpya wa Kielektroniki ulioboreshwa (PlanRep) yanayofanyika mjini Dodoma yakiwashirikisha Waganga Wakuu wa Mikoa, Halmashauri, Maafisa Mipango, Makatibu wa Afya, Wachumi na Wahasibu.[/caption]

Beatrice  Lyimo- Maelezo,Dodoma

Watendaji wa wa Serikali  wametakiwa kufanya kazi kwa kujituma na weledi ili kuendana na dhana ya Serikali ya awamu ya Tano inayosisitiza uwazi  na uwajibikaji katika kuwahudumia wananchi katika maeneo yakutolea huduma.

Akizungumza wakati  akifungua mafunzo  kwa watumiaji wa mfumo wa kielektroniki wa kuandaa Mipango,Bajeti na Ripoti  (PlanRep)za Mamlaka za Serikali za Mitaa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bibi Rehema Madenge amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kuongeza tija katika kuwahudumia wananchi.

[caption id="attachment_10684" align="aligncenter" width="750"] Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Bw. Erick Kitali akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa mafunzo hayo.[/caption]

“Sasa ni lazima watumishi wa umma katika maeneo yakutolea huduma  mbadilike  na muendane na Dhana ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Hapa Kazi  Tu inayosisistiza kutoa huduma bora zinazolenga kuboresha maisha ya wananchi wa chini” Alisisitiza Bi Rehema

Akifafanua  Bi Rehema amesema kuwa matokeo ya matumizi ya mfumo huo ulioboreshwa yanaonekana na yatagusa maisha ya wananchi wote katika maeneo yao kwa kuwa  yatasaidia kuongeza tija na uwajibikaji hali itakayosaidia kuchochea kasi ya ukuaji wa uchumi.

Aliongeza kuwa mfumo wa  PlanRep ulioboreshwa utatumika kuanzia ngazi ya msingi yaani vituo vya kutolea huduma za kijamii ikiwemo  Zahanati,Hospitali na Shule.

[caption id="attachment_10685" align="aligncenter" width="750"] Kiongozi wa Timu ya Mifumo kutoka Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) Bw. Desderi Wengaa akitoa maelezo kuhusu utendaji wa Mfumo huo wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo mjini Dodoma.[/caption]

Mfumo huu wa kuandaa Mipango,Bajeti na Kutoa Ripoti utapunguza gharama kwa kiasi kikubwa zilizokuwa zikitumika awali kabla ya kuanza kwa mfumo huu mpya.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Timu ya Mifumo ya TEHAMA kutoka mRadi wa PS3  Desderi  Wengaa amesema kuwa lengo la mradi huu ni Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) unatakekelezwa na Serikali ya Tanzania ukilenga kuimarisha Mifumo katika Sekta ya Umma ili kuboresha utoaji wa huduma za Serikali za Mitaa kwa Jamii hasa zile zenye uhitaji zaidi.

“Mradi huu unafanya kazi katika maeneo makuu matano ambayo ni Utawala Bora, Ushirikishwaji wananchi, Rasilimali watu, Rasilimali Fedha, Mifumo ya TEHAMA pamoja na Tathimini na ufutiliaji” alisema Desderi Wengaa.

  [caption id="attachment_10687" align="aligncenter" width="750"] Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bibi Rehema Madenge akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo mara baada ya hafla ya ufunguzi. (Picha zote na Frank Mvungi-Maelezo Dodoma).[/caption]

Kiongozi huyo aliongeza kuwa, mfumo huu umesukwa na wataalamu wazalendowa hapa nchini na upo tayari kupokea mabadiliko kulingana na mahitaji ya wakati, na vilevile  utasaidia kupunguza muda na gharama za uaandaaji wa Mipango na Bajeti.

Mradi wa uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma(PS3) ni mradi wa miaka mitano ulia mnamo Julai 2015 na kutarajiwa kukamilika Julai 2020 ambapo utarahisisha utendaji kazi na kusaidia kutatua changamoto zilizokuwepo awali.

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi