Na Mwandishi wetu, Dar
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya watu wa China zimeahidi kuendeleza ushirikiano wa kidiplomasia baina ya nchi hizo kwa kuzingatia misingi ya ushirikiano wa kirafiki kwa maslahi mapana ya mataifa yote mawili.
Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) alipokutana kwa mazungumzo na Balozi wa China nchini, Mhe. Chen Mingjian katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.
Waziri Mulamula amesema katika mazungumzo yao wamejadili masuala mbalimbali, ikiwemo suala la namna ya kuimarisha misingi ya ushirikiano baina ya mataifa hayo.
Pages: 1 2