Na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya ameitaka menejimenti na viongozi wa taasisi wa Sekta ya Uchukuzi kufanya maamuzi ili kutochelewesha maendeleo kwa wananchi katika utekelezaji wa miradi.
Ametoa kauli hiyo wakati akifunga mkutano wa siku mbili wa baraza la Wafanyakazi la sekta ya Uchukuzi lililofanyika mkoani Mwanza na kusema kuwa awamu hii imejikita katika matokeo na sio mazoea.
“Katika awamu hii watendaji wengi wamekuwa wakichelewa kutoa maamuzi katika maeneo mbalimbali sababu ya kutojiamini hii inafanya utekelezaji wa miradi kuchelewa kukamilika na kuchelewesha maendeleo kwa wananchi” amesema Mhandisi Kasekenya.
Pages: 1 2