- Na Mwandishi maalum – Dar es Salaam
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) itawahudumia wagonjwa wenye matatizo ya moyo yanayohitaji matibabu ya kibingwa walioko katika kituo cha watu waliopata maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Corona (COVID – 19) cha Amana jijini Dar es Salaam.
Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Janabi alipotembelea kituo hicho kwa ajili ya kuona ni namna gani wataalamu wa Taasisi yake wataweza kutoa huduma kwa wagonjwa wa moyo.
Prof. Janabi alisema licha ya Taasisi hiyo kwenda katika kituo hicho kutoa huduma ya matibabu ya kibingwa ya moyo pia itatoa mafunzo kwa vikundi vya watu wachache kwa wafanyakazi wa Hospitali hiyo ambayo yatawasaidia katika utendaji wao wa kazi wa kila siku hasa katika kipindi hiki cha janga la Corona.
“Mimi pamoja na wataalamu wangu tumekuja hapa ili kuona ni jinsi gani tunaweza kushirikiana kwa pamoja katika kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa wagonjwa. Kwani wagonjwa wa Corona ambao wanamatatizo ya moyo wanahitaji kupata huduma za matibabu walizokuwa wanazipata kabla hawajapata maambukizi”,.
“Pia tutatoa mafunzo katika makundi ya watu wachache kwa wataalamu wa afya ya jinsi ya kutoa huduma kwa wagonjwa hasa wenye matatizo ya moyo”, alisema Prof. Janabi.
Kwa upande wake Dkt. Stanley Binagi ambaye ni msimamizi wa kituo hicho alisema baadhi ya wagonjwa waliopo katika kituo cha Amana wanasumbuliwa na magonjwa mengine ikiwepo moyo, figo na kisukari yanayohitaji matibabu ya kibingwa .
“Ninawashukuru Wataalamu kutoka JKCI na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambao mmefika katika kituo hiki na kuona jinsi gani mnaweza kushirikiana na sisi katika kutoa huduma za matibabu ya kibingwa kwa wagonjwa wa COVID -19”.
“Kupatikana kwa huduma za matibabu kutoka kwa wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuokoa maisha ya wagonjwa hawa”, alisema Dkt. Binagi.
Undeniably believe that which you stated. Your favorite reason appeared to be on the web the easiest thing to be aware of.
I say to you, I definitely get annoyed while people
consider worries that they plainly don’t know about. You
managed to hit the nail upon the top and defined out the whole thing without having side effect ,
people can take a signal. Will likely be back to get more.
Thanks
Excellent post however I was wanting to know if you could write a litte more on this subject?
I’d be very grateful if you could elaborate a little bit more.
Kudos!
That is really attention-grabbing, You are a very professional blogger.
I have joined your rss feed and look ahead to seeking more of your excellent post.
Also, I have shared your website in my social networks
It’s really a nice and useful piece of info. I am
happy that you just shared this helpful information with us.
Please keep us up to date like this. Thanks for sharing.
tindr , tinder website https://tinderdatingsiteus.com/