Karibuni kwenye Blogu Rasmi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Huu ni Uwanja wa Wananchi Kupata Taarifa Mbalimbali za Serikali na Masuala Mengine ya Kijamii, Kisiasa, na Kiuchumi. Blogu hii inaratibiwa na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali kupitia Idara ya Habari (MAELEZO).
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akiongea alipokuwa akiwasilisha makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi ya fedha ya wizara hiyo kwa mwaka 2022/23 leo Mei 20, 2022, bungeni Jijini Dodoma.
Idara ya Habari – MAELEZO imekusanya jumla ya shilingi 354,190,750 sawa na asilimia 199 katika mwaka wa fedha 2021/2022.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema hayo leo Mei 20, 2022, bungeni Jijini Dodoma alipokuwa akiwasilisha makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka 2022/23 ya wizara hiyo.
“Idara ya Habari – MAELEZO ilikadiriwa kukusanya kiasi cha shilingi 178,017,222 kutokana na mauzo ya picha za viongozi Wakuu wa Nchi na picha ya Baba wa Taifa, vitambulisho, machapisho na ada ya mwaka ya magazeti. Hadi kufikia Aprili 30, 2022, Idara imekusanya jumla ya shilingi 354,190,750 ambayo ni sawa na asilimia 199,” alifafanunua Nnauye.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye alipokuwa akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Na Ahmed Sagaff
Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imekadiria kutumia shilingi bilioni 3.3 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kuendeleza Ubunifu na Utengenezaji wa Vifaa vya TEHAMA katika Mwaka wa Fedha 2022/23.
Hayo yameelezwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye alipokuwa akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akiwa bungeni leo jijini Dodoma wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti ya wizara hiyo.
Asilimia 69 ya Ardhi inafikiwa na Mawasiliano ya Simu za Kiganjani
Na. Georgina Misama – MAELEZO, Dar es Salaam
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Sekta ya Habari na Mawasiliano nchini imekua kwa kasi ya asilimia 8.4 kwa mwaka 2020 ambapo kumekuwa na ongezeko la upatikanaji na matumizi ya huduma za mawasiliano na kusambaa kwa huduma zitolewazo na Vyombo vya Habari.
Katika hotuba yake ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa mwaka 2022/2023 aliyoitoa leo Mei 20, 2022 Bungeni Dodoma, Waziri Nape amesema kulingana na uchambuzi uliofanywa na Wizara husika mwaka 2021 unaonyesha kwamba hivi sasa asilimia 69 ya ardhi ya Tanzania inafikiwa na huduma ya mawasiliano ya simu za kiganjani ambapo kumekuwa na ongezeko la usajili wa laini za simu, watumiaji wa intaneti na watumiaji wa huduma ya kutuma na kupokea fedha.
“ Takwimu zinaonyesha kuwa laini za simu zilizosajiliwa kutoka mwezi Aprili 2021 zimeongezeka kwa asilimia 4.5, watumiaji wa intaneti wameongezeka kutoka milioni 29.1 Aprili, 2021 hadi kufikia milioni 29.9 Aprili 2022 sawa na ongezeko la asilimia 2.7, lakini pia watumiaji wa huduma za kutuma na kupokea pesa kwa njia ya simu wameongezeka kwa asilimia 30.8,” alisema Waziri Nape.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye akijibu baadhi ya hoja zilizokuwa zikitolewa na Wabunge baada ya kumaliza kuwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara yake leo Bungeni.
Na Judith Mhina – Maelezo
Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) waunganisha Tanzania kwa kuongeza huduma ya minara ya mitandao Bara na Zanzibar kwa kujenga minara 181 passive part ambapo imekamilika, minara hiyo inakadiriwa kuwashwa kabla ya mwezi Oktoba 2022.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye ameyasema hayo leo wakati wa kuwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara yake leo Bungeni.
Akiwasilisha Hotuba hiyo, Waziri Nape amesema “ Serikali imeweza kuingia makubaliano na watoa huduma 161 wa Bara na visiwani, na minara hii itajengwa mipakani maeneo ya ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri ambazo zilikuwa hazina huduma za Mawasiliano”
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Khamis Hamza Khamis akizungumza wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Sekta ya Mazingira na Maliasili uliofanyika katika Ukumbi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Mei 20, 2022.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja akitoa neno wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Sekta ya Mazingira na Maliasili uliofanyika katika Ukumbi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Mei 20, 2022.
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Pauline Gekul akizungumza na Uongozi wa Chama cha Netiboli nchini (CHANETA) (hawapo pichani) leo Mei 20, 2022 Dodoma walipofika kujitambulisha kwake mara baada ya kufanya uchaguzi.
Na Shamimu Nyaki – WUSM, Dodoma
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Pauline Gekul ameliagiza Baraza la Michezo Tanzania ( BMT) kuhakikisha Chama Cha Mpira wa Miguu Wanawake nchini (TWFF) kinafanya uchaguzi ili wanawake wanaoshiriki michezo wapate uongozi utakaosaidia kuendesha michezo ya kundi hilo.
Naibu Waziri ametoa agizo hilo leo Mei 20, 2022 alipokutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) uliofika kujitambulisha kwa Naibu Waziri baada ya kufanya uchaguzi kwa ukamilifu.
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Pauline Gekul ameuagiza uongozi wa Chama Cha Netiboli nchini (CHANETA) ufike katika Mikoa na Halmashauri zote nchini ili kuibua vipaji vya mchezo huo.
Naibu Waziri Gekul ametoa agizo hilo leo Mei 20, 2022 jijini Dodoma alipokutana na kufanya mazungumzo na uongozi mpya uliofika kujitambulisha kwa Naibu Waziri baada ya kufanya uchaguzi kwa ukamilifu.
“Hongereni sana wa kufanya uchaguzi, Wizara tupo tayari kushirikiana na nyie katika kuendeleza netiboli nchini, na nawaahidi wizara itakutana na nyie kuona mpango mkakati wenu wa kuendeleza mchezo huu,” alisema Naibu Waziri Gekul.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb) akizungumza leo jijini Dodoma wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo.
Na Mawazo Kibamba, MAELEZO
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb) amesema hadi kufikia tarehe Aprili 30, 2022 jumla ya anwani za makazi 12,171,320 zimekusanywa na kuingizwa kwenye Programu tumizi ikiwa ni sawa na asilimia 104.3 ya lengo la jumla ya Anwani 11,676,891 zilizopangwa kukusanywa katika Mikoa yote nchini.
Ameyasema hayo leo Mei 20, 2022 Bungeni Jijini Dodoma alipokuwa akiwasilisha makadirio ya bajeti ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha 2022/2023 ya Wizara hiyo.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye alipokuwa akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mei 20, 2022 jijini Dodoma.
Na Ahmed Sagaff
Serikali imepanga kutumia shilingi bilioni 39.3 kutekeleza mradi wa Tanzania ya kidijiti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 utakaoanza Julai 2022 ambao utakuza Uchumi wa Kidijitali.
Hayo yameelezwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye alipokuwa akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri Nape amesema fedha hizo zitatumika kujenga kituo kimoja cha kukuza taaluma na ubunifu katika TEHAMA na vituo vidogo vitano kwenye kila Kanda, kukarabati vituo 10 vya Huduma pamoja na kutekeleza programu ya uelimishaji umma kuhusu mradi.